SUMAJKT Chang'ombe Furniture Co Ltd.

Kiwanda hiki kilinunuliwa na JKT tangu mwaka 1972 kama kiwanda kidogo cha kuzalisha samani na kukabidhiwa SUMAJKT mwaka 1982 kwa ajili ya mafunzo ya vijana na uzalishaji kibiashara.

Baada ya maboresho, kiwanda hiki kilisajiliwa mnamo tarehe 12 Machi 2020 kuwa kampuni kwa jina la “SUMAJKT Chang’ombe Furniture Co. Ltd”. Kiwanda kinamilikiwa na Shirika kwa asilimia mia moja.

Lengo letu ni kutengeneza samani bora kwa ajili ya taasisi za Serikali, mashirika ya umma, makampuni na watu binafsi.

Uzoefu Wa Kampuni

  • Tunajivunia umahiri na weledi katika kutengeneza
    bidhaa zetu.
  • Kuchanganya ubunifu, ufundi na teknolojia ili
    kubuni samani zinazofaa kwa wateja wote.
  • Kwa samani za nyumbani, ofisini na shuleni, tuna
    suluhisho kwa wateja wetu wote wa ndani na nje ya
    nchi.
  • Tunazingatia kutoa huduma nzuri kwa wateja,
    ubunifu wa samani kulingana na thamani ya fedha.
    Hizi inatuwezesha kuaminiwa na wateja wetu.

Malengo ya Kampuni

  • Kuwa wauzaji bora wa Samani za nyumbani,
    ofisini na shuleni nchini.
  • Kudumisha ubora katika kila bidhaa.
  • Baada ya huduma za mauzo, tunaamini na
    kuthamini mahusiano mazuri na wateja wetu.
  • Ukaguzi wa kiufundi na huduma ni sehemu
    muhimu sana ya huduma zetu.

Maono ya Kampuni

Kuwa watengenezaji wa samani nchini, kutoa
huduma bora zaidi na ubunifu wa samani
mbalimbali.

Mipango ya Kampuni

Kuzalisha bidhaa zenye ubora wa hali ya juu na kwa wakati.

Tunazingatia mahitaji yawateja kupitia ubunifu wa
Samani na kwa gharama nafuu

Fanya kazi nasi leo

Mkabala na Jengo la NHC Keko

Simu: +255733768893 / +255733768893

P O Box 5268 Dar es salaam

E-mail: sumajktfurniture@mail.com