SUMAJKT Anit Asfalt Co. Ltd

Hii ni kampuni ya ubia kati ya SUMAJKT na kampuni ya ANIT ASFALT kutoka nchini Uturuki. Shirika liliingia ubia na kampuni hiyo tarehe 07 Novemba 2015 kwa makubaliano ya kusaga na kuuza kokoto.

Kampuni inaendelea na uzalishaji wa kokoto katika eneo la Pongwe Msungura Mkoani Pwani.

kokoto

Kuanzishwa

Mradi upo eneo la Mwenge Jijini Dar es Salaam. Mradi huu ni matokeo ya juhudi za Serikali zilizofanywa katika kutekeleza mpango wa kuinua sekta ya kilimo kupitia kauli mbiu ya “Kilimo Kwanza” mwaka 2009 kutokana na juhudi za Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
na Amiri Jeshi Mkuu.

Shirika katika mpango huo lilipewa jukumu la kupokea kutoka Serikalini na kusambaza matrekta na zana za kilimo zilizonunuliwa kutoka nje.

Hivyo, JKT kupitia Shirika lilianzisha mradi wa matrekta ili kutekeleza jukumu hilo la Serikali.

Shughuli zetu

Kampuni inachakata miamba ya ardhini iliyopo eneo la Msata ambayo imesheheni madini ya granite  ambayo hutumika katika kutengeneza kokoto za maumbo mbalimbali kwa ajili ya miradi ya ujenzi wa barabara za lami, ujenzi wa majengo ya serikali na binafsi.

kokoto

Orodha ya Bidhaa zetu


▪ Mchanga wa size 0-5mm.
▪ Kokoto za lami na za kawaida size 5-14 mm.
▪ Kokoto za lami na ka kawaida za size 14-20 mm.
▪ Kokoto za kawaida 20-25 mm.
▪ Mawe ya size kati ya 200-500mm
▪ CRR za size 0-30mm
▪ CRS za size 0-30mm

Fanya kazi nasi leo

Kwa huduma bora ya kokoto za aina zote, mchanga na mawe kwa ajili ya ujenzi, usisite kuwasiliana nasi kupitia njia hizi:

P.O . BOX 5354,
Dar Es Salaam, Tanzania.

Simu/WhatsApp: +255 782 088 998 / +255 755 431 661

email: info@sumajktanit.co.tz

au fika Makao Makuu ya SUMAJKT Anit Asfalt, Pongwe, kijiji cha Msungura, Pwani.